Jeremiah 4:1-6

1 a“Ikiwa utataka kurudi, ee Israeli,
nirudie mimi,”
asema Bwana.
“Ikiwa utaondoa sanamu zako za kuchukiza mbele ya macho yangu
na usiendelee kutangatanga,

2 bikiwa kwa kweli, kwa haki na kwa unyofu utaapa,
‘Kwa hakika kama vile Bwana aishivyo,’
ndipo mataifa yatakapobarikiwa naye
na katika yeye watajitukuza.”

3 cHili ndilo asemalo Bwana kwa watu wa Yuda na kwa Yerusalemu: “Vunjeni mabonge kwenye mashamba yenu,
wala msipande katikati ya miiba.

4 dJitahirini katika Bwana,
tahirini mioyo yenu,
enyi wanaume wa Yuda
na watu wa Yerusalemu,
la sivyo ghadhabu yangu itatoka kwa nguvu
na kuwaka kama moto
kwa sababu ya uovu mliotenda,
ikiwaka pasipo wa kuizima.

Maafa Kutoka Kaskazini


5 “Tangaza katika Yuda na upige mbiu katika Yerusalemu na kusema:
‘Piga tarumbeta katika nchi yote!’
Piga kelele na kusema:
‘Kusanyikeni pamoja!
Tukimbilie katika miji yenye maboma!’

6 eOnyesheni ishara ili kwenda Sayuni!
Kimbilieni usalama pasipo kuchelewa!
Kwa kuwa ninaleta maafa kutoka kaskazini,
maangamizi ya kutisha.”

Copyright information for SwhKC